Zaburi 142
Maombi ya kuokolewa dhidi ya watesi
Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi.
Namlilia Mwenyezi Mungu kwa sauti,
napaza sauti yangu kwa Mwenyezi Mungu anihurumie.
Namimina malalamiko yangu mbele zake,
mbele zake naeleza shida zangu.
 
Roho yangu inapozimia ndani yangu,
wewe ndiwe unajua njia zangu.
Katika njia ninayopita,
watu wameniwekea mtego.
Tazama kuume kwangu na uone,
hakuna hata mmoja anayejihusisha nami.
Sina kimbilio,
hakuna anayejali maisha yangu.
 
Ee Mwenyezi Mungu, nakulilia wewe,
nasema, “Wewe ni kimbilio langu,
fungu langu katika nchi ya walio hai.”
Sikiliza kilio changu,
kwa sababu mimi ni mhitaji sana;
niokoe na wale wanaonifuatilia,
kwa kuwa wamenizidi nguvu.
Nifungue kutoka kifungo changu,
ili niweze kulisifu jina lako.
 
Ndipo wenye haki watanizunguka,
kwa sababu ya wema wako kwangu.