Zaburi 6
Sala ya kuomba msaada wakati wa taabu 
 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi.*Sheminithi ni mtajo mmojawapo katika lugha ya uimbaji. Zaburi ya Daudi. 
  1 Ee Mwenyezi Mungu, usinikemee katika hasira yako,  
wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.   
 2 Unirehemu Mwenyezi Mungu,  
kwa maana nimedhoofika;  
Ee Mwenyezi Mungu, uniponye,  
kwa maana mifupa yangu  
ina maumivu makali.   
 3 Nafsi yangu ina uchungu mwingi.  
Hadi lini, Ee Mwenyezi Mungu, hadi lini?   
 4 Geuka, Ee Mwenyezi Mungu, unikomboe,  
uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.   
 5 Hakuna mtu anayekukumbuka  
akiwa amekufa.  
Ni nani awezaye kukusifu  
 6 Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni;  
usiku kucha natiririsha  
kitanda changu kwa machozi;  
nimelowesha kiti changu  
kwa machozi yangu.   
 7 Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika,  
yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.   
 8 Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya,  
kwa maana Mwenyezi Mungu amesikia kulia kwangu.   
 9 Mwenyezi Mungu amesikia kilio changu kwa huruma,  
Mwenyezi Mungu amekubali sala yangu.   
 10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika,  
watarudi nyuma na waaibishwe kwa ghafula.   
*^ Sheminithi ni mtajo mmojawapo katika lugha ya uimbaji.
†Zaburi 6:5 Kuzimu kwa Kiebrania ni Sheol, yaani Shimo lisilo na mwisho.