Zaburi 70
Kuomba msaada
(Zaburi 40:13-17)
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Maombi.
1 Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa;
Ee Mwenyezi Mungu, njoo hima unisaidie.
2 Wale wanaotafuta kuniua,
waaibishwe na kufadhaishwa;
wote wanaotamani kuangamizwa kwangu,
warudishwe nyuma kwa aibu.
3 Wale wanaoniambia, “Aha! Aha!”
na warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.
4 Lakini wote wanaokutafuta
washangilie na kukufurahia,
wale wanaoupenda wokovu wako siku zote waseme,
“Mwenyezi Mungu ni mkuu!”
5 Lakini mimi bado ni maskini na mhitaji;
Ee Mungu, unijie haraka.
Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu;
Ee Mwenyezi Mungu, usikawie.