17
Ni bora kuwa na utulivu pamoja chembe za mkate kuliko nyumba yenye sherehe nyingi pamoja na ugomvi. Mtumishi mwenye busara atatawala juu ya mwana atendaye kwa aibu na atashiriki urithi kama mmoja wa ndugu. Kalibu ni kwa fedha na tanuu ni kwa dhahabu, bali Yehova huisafisha mioyo. Mtu atendaye mabaya huwasikiliza wale wanaosema maovu; muongo anausikivu kwa wale wanaosema mambo mabaya. Mwenye kumdhihaki masikini humtukana Muumba wake na anayefurahia msiba hatakosa adhabu. Wajukuu ni taji ya wazee na wazazi huleta heshima kwa watoto wao. Hotuba ya ushawishi haifai kwa mpumbavu; kidogo zaidi midomo ya uongo inafaa kwa ufalme. Rushwa ni kama jiwe la kiini macho kwa yule ambaye atoaye; yeye anayeiacha, hufanikiwa. Anayesamehe kosa hutafuta upendo, bali yeye anayerudia jambo huwatenganisha marafiki wa karibu. 10 Karipio hupenya ndani ya mtu mwenye ufahamu kuliko mapigo mamia kwenda kwa mpumbavu. 11 Mtu mbaya hutafuta uasi tu, hivyo mjumbe katiri atatumwa dhidi yake. 12 Ni bora kukutana na dubu aliyeporwa watoto wake kuliko kukutana na mpumbavu katika upumbavu wake. 13 Mtu anaporudisha mabaya badala ya mema, mabaya hayatatoka katika nyumba yake. 14 Mwanzo wa mafarakano ni kama mtu anayefungulia maji kila mahali, hivyo ondoka kwenye mabishano kabla ya kutokea. 15 Yeye ambaye huwaachilia watu waovu au kuwalaumu wale wanaotenda haki - watu hawa wote ni chukizo kwa Yehova. 16 Kwa nini mpumbavu alipe fedha kwa kujifunza hekima, wakati hana uwezo wa kujifunza? 17 Rafiki hupenda kwa nyakati zote na ndugu amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu. 18 Mtu asiyekuwa na akili hufanya ahadi zenye mashariti na kuanza kuwajibika kwa madeni ya jirani yake. 19 Apendaye mafarakano anapenda dhambi; ambaye hutengeneza kizingiti kirefu sana kwenye mlango wake husababisha kuvunjia kwa mifupa. 20 Mtu mwenye moyo wa udanganyifu hapati chochote ambacho ni chema; na mwenye ulimi wa ukaidi huanguka kwenye janga. 21 Mzazi wa mpumbavu huleta majonzi kwake mwenyewe; baba wa mpumbavu hana furaha. 22 Moyo mchangamfu ni dawa njema, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa. 23 Mtu mwovu hukubali rushwa ya siri ili kupotosha njia za haki. 24 Mwenye ufahamu huelekeza uso wake kwenye hekima, bali macho ya mpumbavu huelekea ncha za dunia. 25 Mwana mpumbavu ni huzuni kwa baba yake na uchungu kwa mwanamke aliyemzaa. 26 Pia, si vizuri kumwadhibu mwenye kutenda haki; wala si vema kuwachapa mjeledi watu waadilifu wenye ukamilifu. 27 Mwenye maarifa hutumia maneno machache na mwenye ufahamu ni mtulivu. 28 Hata mpumbavu hudhaniwa kuwa na busara kama akikaa kimya; wakati anapokaa amefunga kinywa chake, anafikiriwa kuwa na akili.