7
Sadaka za kuweka wakfu Maskani ya Mwenyezi Mungu
Musa alipomaliza kuisimamisha Maskani, aliipaka mafuta na kuiweka wakfu pamoja na samani zake zote. Pia alitia madhabahu mafuta na kuiweka wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote. Ndipo viongozi wa Israeli, wale wakuu wa jamaa waliokuwa viongozi wa kabila wasimamizi wa wale waliohesabiwa, wakatoa sadaka. Walizileta kama matoleo yao mbele za Mwenyezi Mungu: magari sita ya kukokotwa yaliyofunikwa, pamoja na maksai kumi na wawili; yaani maksai mmoja kutoka kwa kila kiongozi, na gari moja la kukokotwa kutoka kwa kila viongozi wawili. Haya waliyaleta mbele ya Maskani.
Mwenyezi Mungu akamwambia Musa, “Vikubali vitu hivi kutoka kwao, ili viweze kutumika katika kazi kwenye Hema la Kukutania. Wapatie Walawi kama kazi ya kila mtu itakavyohitaji.”
Hivyo Musa akachukua yale magari ya kukokotwa pamoja na maksai, na kuwapa Walawi. Aliwapa Wagershoni magari mawili ya kukokotwa na maksai wanne, kama walivyohitaji kwa kazi yao, na pia aliwapa Wamerari magari manne ya kukokotwa na maksai wanane, kama kazi yao ilivyohitaji. Wote walikuwa chini ya maelekezo ya Ithamari mwana wa kuhani, Haruni. Lakini Musa hakuwapa Wakohathi chochote kati ya hivyo, kwa sababu walitakiwa kubeba vitu vitakatifu mabegani mwao, vile walikuwa wanawajibika.
10 Madhabahu yalipopakwa mafuta, viongozi walileta sadaka zao kwa ajili ya kule kuwekwa wakfu kwake na kuziweka mbele ya madhabahu. 11 Kwa maana Mwenyezi Mungu alikuwa amemwambia Musa, “Kila siku kiongozi mmoja ataleta sadaka yake ili kuwekwa wakfu madhabahu.”
 
12 Yule ambaye alileta sadaka yake siku ya kwanza alikuwa Nashoni, mwana wa Aminadabu, wa kabila la Yuda.
13 Sadaka yake ilikuwa:
sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli mia moja na thelathini*Shekeli 130 za fedha ni sawa na kilo 1.5., na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabiniShekeli 70 za fedha ni sawa gramu 800., vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya nafaka;
14 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumiShekeli 10 za dhahabu ni sawa na gramu 110., likiwa limejazwa uvumba;
15 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
16 beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
17 maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani.
Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Nashoni mwana wa Aminadabu.
 
18 Siku ya pili yake Nethaneli mwana wa Suari, kiongozi wa Isakari, alileta sadaka yake.
19 Sadaka aliyoleta ilikuwa:
sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli mia moja na thelathini, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya nafaka;
20 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
21 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
22 beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
23 maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani.
Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Nethaneli mwana wa Suari.
 
24 Siku ya tatu Eliabu mwana wa Heloni, kiongozi wa watu wa Zabuloni, alileta sadaka yake.
25 Sadaka aliyoleta ilikuwa:
sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli mia moja na thelathini, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya nafaka;
26 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
27 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
28 beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
29 maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani.
Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Eliabu mwana wa Heloni.
 
30 Siku ya nne Elisuri mwana wa Shedeuri, kiongozi wa watu wa Reubeni, alileta sadaka yake.
31 Sadaka aliyoleta ilikuwa:
sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli mia moja na thelathini, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya nafaka;
32 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
33 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
34 beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
35 maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani.
Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Elisuri mwana wa Shedeuri.
 
36 Siku ya tano Shelumieli mwana wa Surishadai, kiongozi wa watu wa Simeoni, alileta sadaka yake.
37 Sadaka aliyoleta ilikuwa:
sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli mia moja na thelathini, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya nafaka;
38 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
39 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
40 beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
41 maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani.
Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Shelumieli mwana wa Surishadai.
 
42 Siku ya sita Eliasafu mwana wa Deueli, kiongozi wa watu wa Gadi, alileta sadaka yake.
43 Sadaka aliyoleta ilikuwa:
sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli mia moja na thelathini, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya nafaka;
44 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
45 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
46 beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
47 maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani.
Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Eliasafu mwana wa Deueli.
 
48 Siku ya saba Elishama mwana wa Amihudi, kiongozi wa watu wa Efraimu, alileta sadaka yake.
49 Sadaka aliyoleta ilikuwa:
sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli mia moja na thelathini, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya nafaka;
50 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
51 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
52 beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
53 maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani.
Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Elishama mwana wa Amihudi.
 
54 Siku ya nane Gamalieli mwana wa Pedasuri, kiongozi wa watu wa Manase, alileta sadaka yake.
55 Sadaka aliyoleta ilikuwa:
sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli mia moja na thelathini, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya nafaka;
56 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
57 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
58 beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
59 maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani.
Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Gamalieli mwana wa Pedasuri.
 
60 Siku ya tisa Abidani mwana wa Gideoni, kiongozi wa watu wa Benyamini, alileta sadaka yake.
61 Sadaka aliyoleta ilikuwa:
sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli mia moja na thelathini, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya nafaka;
62 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
63 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
64 beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
65 maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani.
Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Abidani mwana wa Gideoni.
 
66 Siku ya kumi Ahiezeri mwana wa Amishadai, kiongozi wa watu wa Dani, alileta sadaka yake.
67 Sadaka aliyoleta ilikuwa:
sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli mia moja na thelathini, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya nafaka;
68 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
69 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
70 beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
71 maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani.
Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Ahiezeri mwana wa Amishadai.
 
72 Siku ya kumi na moja Pagieli mwana wa Okrani, kiongozi wa watu wa Asheri, alileta sadaka yake.
73 Sadaka aliyoleta ilikuwa:
sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli mia moja na thelathini, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya nafaka;
74 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
75 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
76 beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
77 maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani.
Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Pagieli mwana wa Okrani.
 
78 Siku ya kumi na mbili Ahira mwana wa Enani, kiongozi wa watu wa Naftali, alileta sadaka yake.
79 Sadaka aliyoleta ilikuwa:
sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli mia moja na thelathini, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya nafaka;
80 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
81 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
82 beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
83 maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani.
Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Ahira mwana wa Enani.
 
84 Hizi ndizo sadaka zilizotolewa na viongozi wa Israeli madhabahu yalipowekwa wakfu, wakati yalipakwa mafuta:
sahani kumi na mbili za fedha, bakuli kumi na mbili za fedha za kunyunyizia, na masinia kumi na mawili ya dhahabu. 85 Kila sahani ya fedha ilikuwa na uzito wa shekeli mia moja na thelathini, na kila bakuli la fedha la kunyunyizia lilikuwa na uzito wa shekeli sabini. Masinia yote kumi na mawili yalikuwa na uzito wa shekeli elfu mbili na mia nne§Shekeli 2,400 za fedha ni sawa na kilo 28. kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. 86 Sahani kumi na mbili za dhahabu zilizojazwa uvumba zilikuwa na uzito wa shekeli kumi kila moja, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. Kwa jumla, sahani za dhahabu zilikuwa na uzito wa shekeli mia moja na ishirini*Shekeli 120 za dhahabu ni sawa na kilo 1.4..
87 Jumla ya wanyama waliotolewa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa walikuwa fahali kumi na wawili wachanga, kondoo dume kumi na wawili, na wana-kondoo dume kumi na wawili wa mwaka mmoja, pamoja na sadaka zao za nafaka. Beberu kumi na wawili walitolewa kwa ajili ya sadaka za dhambi.
88 Jumla ya wanyama kwa ajili ya dhabihu ya sadaka ya amani walikuwa maksai ishirini na wanne, kondoo dume sitini, beberu wa mwaka mmoja sitini, na wana-kondoo dume wa mwaka mmoja sitini.
 
Hizo ndizo sadaka zilizoletwa kwa ajili ya kuwekwa wakfu kwa madhabahu baada ya kupakwa mafuta.
 
89 Musa alipoingia kwenye Hema la Kukutania kuzungumza na Mwenyezi Mungu, alisikia sauti ikisema naye kutoka kati ya wale makerubi wawili waliokuwa juu ya kile kiti cha rehema, juu ya Sanduku la Ushuhuda. Musa akazungumza na Mwenyezi Mungu.

*7:13 Shekeli 130 za fedha ni sawa na kilo 1.5.

7:13 Shekeli 70 za fedha ni sawa gramu 800.

7:14 Shekeli 10 za dhahabu ni sawa na gramu 110.

§7:85 Shekeli 2,400 za fedha ni sawa na kilo 28.

*7:86 Shekeli 120 za dhahabu ni sawa na kilo 1.4.