*Katika nakala za kale za Kiebrania, Zaburi 42 na 43 ni moja
Zaburi 43
Maombi ya mtu aliye uhamishoni yanaendelea
Ee Mungu unihukumu,
nitetee dhidi ya taifa lisilomcha Mungu,
niokoe na watu wadanganyifu na waovu.
Wewe ni Mungu ngome yangu.
Kwa nini umenikataa?
Kwa nini niendelee kuomboleza,
nikidhulumiwa na adui?
Tuma hima nuru yako na kweli yako viniongoze;
na vinilete hadi mlima wako mtakatifu,
mahali unapoishi.
Ndipo nitaenda madhabahuni pa Mungu,
kwa Mungu, furaha yangu na shangwe yangu.
Nitakusifu kwa kinubi,
Ee Mungu, Mungu wangu.
 
Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?
Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?
Weka tumaini lako kwa Mungu,
kwa sababu bado nitamsifu
Mwokozi wangu na Mungu wangu.

*^ Katika nakala za kale za Kiebrania, Zaburi 42 na 43 ni moja