Zaburi 110
Mwenyezi Mungu na mfalme wake mteule 
 Zaburi ya Daudi. 
  1 Mwenyezi Mungu amwambia Bwana wangu:  
“Keti mkono wangu wa kuume,  
hadi nitakapowafanya adui zako  
kuwa mahali pa kuweka miguu yako.”   
 2 Mwenyezi Mungu ataeneza fimbo yako ya utawala yenye nguvu kutoka Sayuni;  
utatawala katikati ya adui zako.   
 3 Askari wako watajitolea kwa hiari  
katika siku yako ya vita.  
Ukiwa umevikwa fahari takatifu,  
kutoka tumbo la mapambazuko  
utapokea umande wa ujana wako*au vijana wako watakujia kama umande.   
 4 Mwenyezi Mungu ameapa,  
naye hatabadilisha mawazo yake:  
“Wewe ni kuhani milele,  
kwa mfano wa Melkizedeki.”   
 5 Bwana yuko mkono wako wa kuume,  
atawaponda wafalme siku ya ghadhabu yake.   
 6 Atawahukumu mataifa, akilundika mizoga  
na kuwaponda watawala wa dunia nzima.   
 7 Atakunywa maji katika kijito kando ya njia†au Yeye atoaye mtu wa kurithi mwingine atamweka kwenye mamlaka;;  
kwa hiyo atainua kichwa chake juu.   
*Zaburi 110:3 au vijana wako watakujia kama umande
†Zaburi 110:7 au Yeye atoaye mtu wa kurithi mwingine atamweka kwenye mamlaka;