Zaburi 110
Mwenyezi Mungu na mfalme wake mteule
Zaburi ya Daudi.
Mwenyezi Mungu amwambia Bwana wangu:
“Keti mkono wangu wa kuume,
hadi nitakapowafanya adui zako
kuwa mahali pa kuweka miguu yako.”
 
Mwenyezi Mungu ataeneza fimbo yako ya utawala yenye nguvu kutoka Sayuni;
utatawala katikati ya adui zako.
Askari wako watajitolea kwa hiari
katika siku yako ya vita.
Ukiwa umevikwa fahari takatifu,
kutoka tumbo la mapambazuko
utapokea umande wa ujana wako*au vijana wako watakujia kama umande.
 
Mwenyezi Mungu ameapa,
naye hatabadilisha mawazo yake:
“Wewe ni kuhani milele,
kwa mfano wa Melkizedeki.”
 
Bwana yuko mkono wako wa kuume,
atawaponda wafalme siku ya ghadhabu yake.
Atawahukumu mataifa, akilundika mizoga
na kuwaponda watawala wa dunia nzima.
Atakunywa maji katika kijito kando ya njiaau Yeye atoaye mtu wa kurithi mwingine atamweka kwenye mamlaka;;
kwa hiyo atainua kichwa chake juu.

*Zaburi 110:3 au vijana wako watakujia kama umande

Zaburi 110:7 au Yeye atoaye mtu wa kurithi mwingine atamweka kwenye mamlaka;