Zaburi 117
Sifa za Mwenyezi Mungu 
  1 Msifuni Mwenyezi Mungu, enyi mataifa yote;  
mtukuzeni yeye, enyi watu wote.   
 2 Kwa kuwa upendo wake kwetu ni mkuu,  
uaminifu wa Mwenyezi Mungu unadumu milele.  
Msifuni Mwenyezi Mungu.*kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.