Zaburi 131
Kumtegemea Mwenyezi Mungu kwa unyenyekevu 
 Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. 
  1 Moyo wangu hauna kiburi, Ee Mwenyezi Mungu,  
macho yangu hayajivuni;  
sijishughulishi na mambo makuu kunizidi  
wala mambo ya ajabu mno kwangu.   
 2 Lakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;  
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,  
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya  
ndivyo ilivyo nafsi iliyo ndani yangu.   
 3 Ee Israeli, mtumaini Mwenyezi Mungu  
tangu sasa na hata milele.