Zaburi 100
Dunia yote yaitwa kumsifu Mwenyezi Mungu
Zaburi ya shukrani.
Mpigieni Mwenyezi Mungu kelele za shangwe, dunia yote.
Mwabuduni Mwenyezi Mungu kwa furaha;
njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
Jueni kwamba Mwenyezi Mungu ndiye Mungu.
Yeye ndiye alituumba, sisi tu mali yake;
sisi tu watu wake,
kondoo wa malisho yake.
 
Ingieni malangoni mwake kwa shukrani
na katika nyua zake kwa kusifu,
mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
Kwa maana Mwenyezi Mungu ni mwema
na fadhili zake zadumu milele;
uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.