Zaburi 113
Kumsifu Mwenyezi Mungu kwa wema wake 
  1 Msifuni Mwenyezi Mungu.*kwa Kiebrania ni Hallelu Yah; pia 113:9.  
Enyi watumishi wa Mwenyezi Mungu msifuni,  
lisifuni jina la Mwenyezi Mungu.   
 2 Jina la Mwenyezi Mungu na lisifiwe,  
sasa na hata milele.   
 3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake,  
jina la Mwenyezi Mungu linapaswa kusifiwa.   
 4 Mwenyezi Mungu ametukuka juu ya mataifa yote,  
utukufu wake juu ya mbingu.   
 5 Ni nani aliye kama Mwenyezi Mungu, Mungu wetu,  
Yule aliyeketi kwenye kiti cha enzi huko juu,   
 6 ambaye huinama atazame chini  
aone mbingu na nchi?   
 7 Huwainua maskini kutoka mavumbini,  
na kuwanyanyua wahitaji  
kutoka lundo la majivu,   
 8 huwaketisha pamoja na wakuu,  
pamoja na wakuu wa watu wake.   
 9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake,  
akiwa mama watoto mwenye furaha.  
Msifuni Mwenyezi Mungu.