Zaburi 114
Maajabu ya Mwenyezi Mungu wakati Israeli walitoka Misri 
  1 Israeli alipotoka Misri,  
nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,   
 2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,  
Israeli akawa milki yake.   
 3 Bahari ilitazama ikakimbia,  
Yordani ulirudi nyuma,   
 4 milima ilirukaruka kama kondoo dume,  
vilima kama wana-kondoo.   
 5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,  
nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,   
 6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,  
enyi vilima, kama wana-kondoo?   
 7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana,  
mbele za Mungu wa Yakobo,   
 8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji,  
mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.