Zaburi 123
Kuomba rehema
Wimbo wa kwenda juu.
Ninayainua macho yangu kwako,
kwako wewe unayeketi mbinguni kwenye kiti chako cha enzi.
Kama vile macho ya watumwa
yatazamavyo mkono wa bwana wao,
kama vile macho ya mjakazi
yatazamavyo mkono wa bibi yake,
ndivyo macho yetu yamtazamavyo Mwenyezi Mungu, Mungu wetu,
hadi atakapotuhurumia.
 
Uturehemu, Ee Mwenyezi Mungu, uturehemu,
kwa maana tumevumilia dharau nyingi.
Tumevumilia dhihaka nyingi kutoka kwa wenye kiburi,
dharau nyingi kutoka kwa wenye majivuno.