Zaburi 125
Usalama wa watu wa Mwenyezi Mungu 
 Wimbo wa kwenda juu. 
  1 Wale wamtumainio Mwenyezi Mungu ni kama Mlima Sayuni,  
ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.   
 2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,  
ndivyo Mwenyezi Mungu anavyowazunguka watu wake  
sasa na hata milele.   
 3 Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi  
waliyopewa wenye haki,  
ili wenye haki wasije wakatumia  
mikono yao kutenda ubaya.   
 4 Ee Mwenyezi Mungu, watendee mema walio wema,  
wale walio wanyofu wa moyo.   
 5 Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,  
Mwenyezi Mungu atawafukuza pamoja na watenda maovu.  
Amani iwe juu ya Israeli.