Zaburi 134
Wito wa kumsifu Mwenyezi Mungu 
 Wimbo wa kwenda juu. 
  1 Msifuni Mwenyezi Mungu, ninyi nyote watumishi wa Mwenyezi Mungu,  
ninyi mnaotumika usiku ndani ya nyumba ya Mwenyezi Mungu.   
 2 Inueni mikono yenu katika patakatifu  
na kumsifu Mwenyezi Mungu.   
 3 Naye Mwenyezi Mungu, Muumba wa mbingu na dunia,  
awabariki kutoka Sayuni.