Zaburi 134
Wito wa kumsifu Mwenyezi Mungu
Wimbo wa kwenda juu.
1 Msifuni Mwenyezi Mungu, ninyi nyote watumishi wa Mwenyezi Mungu,
ninyi mnaotumika usiku ndani ya nyumba ya Mwenyezi Mungu.
2 Inueni mikono yenu katika patakatifu
na kumsifu Mwenyezi Mungu.
3 Naye Mwenyezi Mungu, Muumba wa mbingu na dunia,
awabariki kutoka Sayuni.